Sunday, 21 February 2010

Wasanii kutoka Monduli nao wamo...



Hawa ni baadhi ya wasanii kutoka Monduli wakiwa wana rekodi mchezo wa redio studioni.Wasanii hawa ambao wamechaguliwa na Mradi wa world vision katika programu yao ARK, wanatunga michezo ya redio nakurekodi.Aidha michezo yao inalenga kuelimisha jamii ya kimasai juu ya Janga la UKIMWI. Makao makuu ya kikundi hiki ni Monduli. Michezo hii hurushwa katika redio zilizo chaguliwa na World Vision, nazo ni Radio ORS,Monduli, Boma Hai FM, Hai na Radio karagwe Bukoba.

Mafunzo ya msingi ya Uandishi na Uigizaji wa michezo ya redio kwa wasanii hawa yali fanywa na Salim Gembe.Aidha katika mafunzo hayo muwezeshaji alichagua wasanii wenye vipaji kwenye maeneo mbali mbali ya sanaa redioni na kuwapa wale wenye vipaji majukuma husika.

No comments:

Post a Comment